wembe ads

wembe ads

Search Posts

Tanzania's Number one gossip blog with latest entertainment news, scandals, fashion and videos. contacts +255 789 120 888 (Dar Es Salaam, Tanzania)

Tuesday, 22 December 2015

FILAMU ZINALIPA, LAKINI SERIKALI YA BONGO INABANA!

Katika wakati kama huu ambapo hali ya maisha imekuwa ngumu, ajira hakuna hasa hapa kwetu Tanzania, tasnia ya filamu au sanaa kwa ujumla inaweza kuwa suluhisho pekee la kupatia ajira mamia ya watanzania hasa vijana! (The... nation, in particular, needs the sector to help rejuvenate hope of better time and faith in the land's ability to ultimately come out of the woods).
“This is my thinking” mimi kama Selles Mapunda, hizo ndizo fikra zangu! Lakini situation hapa nchini kwetu haiku hivyo hasa kwetu sisi wadau wa tasnia hii ya filamu. Serikali yetu chini ya maraisi wote waliopita mpaka leo hii JK haitusaiidii katika misingi inayoweza kutengeneza ajira kwa wasanii. Hapa namaanisha kwamba serikali kujenga misingi itakayo wasaidia wasanii wote sio wale wawili watatu wanaoitwa kwenye kampeni za uchaguzi au wale walio karibu na raisi! Hapa naweza nikasema kwamba mh. Raisi JK na serikali yenu mnaiweka tasnia ya filamu kwenye “situation where the country tends to exploit and wreck the filmmakers' investments without propping them” .
Nilibahatika kufanyiwa interview na mwandishi wa habari za mambo ya filamu za kiafrika toka nchini Marekani kupitia kwenye televisheni ya Chanel ten ya hapa nchini, mimi kama Director na Producer,  mwandishi huyu alitaka kujua nini sisi waandaaji wa filamu wa hapa Tanzania tunafanya kwenye tasnia hii ya filamu hasa katika kipengele cha “Telling stories in a Tanzanian way  about culture and creativity”. Alitaka pia kufahamu filamu zetu zinasaidiaje katika kuwajenga watanzania katika kukuza na kuendeleza mila na desturi za mtanzania, niliongea nae mambo mengi sana lakini moja kati ya mambo makubwa niliyojifunza kwake ni kwamba tasnia ya filamu hapa nchini kama itapata sapoti kutoka serikalini inaweza pia kubadilisha maisha ya watanzania wengi hususani wasanii aliniambia “Bongo movies can be used to solve society's problems, can launch a man from grass to grace”.
Interestingly, mimi binafsi kama director na mshikadau wa Bongo Movies nikavuta picha ya nilikotoka mpaka nilipo kwenye hii tasnia, tangu utoto wangu nilikuwa na mapenzi na tasnia hii, rasmi nilianza kujishughulisha na mambo ya tasnia ya filamu nikiwa na umri wa miaka 14 wakati huo wenzangu wengi walikuwa bado wanabebwa mimi tayari nilikuwa nafuatilia tamthilia za Isidingo na Days of our lives!
 “Nilianza kuigiza nikiwa shule ya msingi miaka ya 80, katika umri huo! Baba yangu hakupenda kabisa mwanawe ajiingize kwenye mambo ya uigizaji au mambo ya sanaa kwa ujumla. Nakumbuka alithubutu kumwambia mama yangu kwamba hataki mwanawe yeyote ajiingize kwenye mambo ya sanaa na hata mambo ya uandishi wa habari na utangazaji, yeye alikuwa siku zote anasema kwamba “artists, journalists and broadcasters do not maintain stable families as they never had the time to spend with their families”.
Hivyo basi alijitahidi kutulazimisha tusome fani nyingine tofauti na sanaa na uandishi wa habari. Kwa bahati mbaya mimi nilipomaliza kidato cha nne, nikajiunga na kidato cha tano na sita nilikosoma combination ya HGL (History, Geography & Language) na baadae kujiunga na chuo kikuu cha UDSM kwenye faculty a Sociology. Mzee Mapunda alijitahidi sana kwa watoto wake wote lakini kwa bahati mbaya kuna usemi wazungu wanapenda sana kuutumia wanasema kwamba “one cannot live out of one's calling and one cannot leave out what one has seen. It is an in-built thing”. Kwamba kufanya shughuli za filamu na uandishi iko kwa damu yangu (is in my blood stream) Hivyo basi kwa mapenzi yangu ya mambo ya sanaa nikaamua kujisomesha mwenyewe kwenye chuo cha sanaa UNILAG kitivo cha uandishi, uongozaji na uzalishaji filamu nchini Nigeria.
Kwa hakika naweza sema kwamba  Im within my line of calling” Yes, kufanya filamu kwangu ni wito,  na ukiangalia leo hii mimi ni mmoja kati ya wadau wakubwa kwenye tasnia ya filamu hapa Tanzania na Afrika kwa ujumla. Mimi ni filmmaker ambae nina taaluma ya uandishi wa miswada ya filamu na uongozaji (writing, and directing) mpaka ninaandika makala hii nimejifunza mambo mengi sana kwenye tasnia hii hususani hapa Tanzania, Nigeria na Ghana. Mwisho wa yote nimegundua kwamba ili kuiendeleza tasnia hii ni lazima wadau tufanye mapinduzi kwa kutengeneza filamu zenye ubora wa kimataifa ili kuzifanya kazi zetu zitambulike kimataifa. (only way we can make an impact in the movie industry is to produce quality films that will bring change).
Nimefanya kazi ya kuandika na kuongoza filamu zaidi ya 30 kupitia kampuni ya usamabazaji wa filamu iitwayo Steps Entertainment ltd, lakini kuna vitu ambavyo kwa kiasi kikubwa kampuni haikuzingatia kuhusu ubora wa filamu inazoandaa na hata kusambaza, nah ii ni kwa sababu kampuni kazi yake kubwa ni kufanya biashara ya kusambaza filamu na sio kuandaa hivyo basi kwa kuliona hili nikaamua rasmi kuanza kuandaa filamu zangu binafsi. Nikaamka tu na kujitamkia kimoyomoyo kwamba “I have to produce my own movies, I have to produce movies for people. I have to direct movies. And, I ran away from those things”.  Nafsini niligundua kwamba namna pekee ya kufanya mabadiliko ni kuandaa filamu zangu kwa kiwango ambacho wapenzi wa filamu hapa Tanzania, Afrika na duniani kote wataelewa ninachokifanya!  Nilijiangalia mwenyewe, nikazipima akili, uwezo na ujuzi nilionao kwenye mambo ya uandaaji wa filamu “it occurred to me that the only way I can make that impact is to produce quality films”.

(story ndiyo kwanza imeanza,unataka kujua nimeandika na kuongoza filamu zipi? Nimefanya kazi na wasanii gani? Usikose sehemu ya pili ya makala hii)

No comments:

Post a Comment