wembe ads

wembe ads

Search Posts

Tanzania's Number one gossip blog with latest entertainment news, scandals, fashion and videos. contacts +255 789 120 888 (Dar Es Salaam, Tanzania)

Tuesday, 22 December 2015

HII NDIYO SABABU YA DIAMOND PLATNUMZ KUTOONEKANA KWENYE PARTY YA ZARI WHITE PARTY 2015 JIJINI KAMPALA NCHINI UGANDA!

Kimenuka!


Zari & Diamond Platinum
Katika hali isiyo ya kawaida kuhusiana na sakata la mahusiano ya kimapenzi baina ya Zari ambaye ni mzazi mwenza wa East African Rolls Royce musician” Diamond Platnumz zamani akifahamika kama Nasib Abdul na mtalaka wa mpenziwe huyo yaani Don Ivan Semwanga kwamba bado hali ni tete kutokana na ukweli kwamba Ivan anaendelea kukana kufahamu uzazi wa mototo wa nne wa bimkubwa Zarina Hassan kwamba baba wa motto huyo ni Diamond! 
Rich Gang
Hii imejirudia majuzi nchini Uganda katika tukio lijulikanalo kama “ZARI ALL WHITE PARTY” ambapo safari hii linadaiwa kusimamiwa na wamiliki wenyewe yaani RICH GANG kundi la matajiri wa Kiganda linaloongozwa na mtalaka wa Zari aitwaye Ivan Semwanga. Katika kuinukisha kile kilichonuka, Ivan alisema katika mahojiano yake na vyombo mbali mbali vya habari nchini humo na kudai kwamba “event” hiyo ni mali ya Rich Gang na Zari huwa anatumwa kuipamba na kuisimamia tu! Wiiki iliyopita ambapo shughuli hiyo ilichukua nafasi jijini Kampala ambapo pia mwanamuziki Diamond Platnumz alikuwapo jijini humo kwa shughuli zake za kimuziki lakini alizuiwa kuungana na mzazi mwenzake yaani Zari katika shughuli hiyo kutokana na kilichodaiwa kuwa ni katazo la Ivan! Ivan anadaiwa kumpiga mkwara Diamond kutokanyaga kwenye party hiyo na kama angeonekana angefukuzwa kama mbwa! Bado kuna utata unaofukuta kwa muda mrefu kuhusiana na hatma ya ndoa kati ya Zari na Ivan, umuliki wa mali zao ambapo mara kadhaa Ivan amejitokeza kwenye vyombo vya habari na kudai kwamba Zari siyo mmiliki wa mali anazoonekana nazo bali ni msimamizi na kudai kwamba yeye Ivan ndiye mmiliki wa mali hizo.Tusubiri

No comments:

Post a Comment