wembe ads

wembe ads

Search Posts

Tanzania's Number one gossip blog with latest entertainment news, scandals, fashion and videos. contacts +255 789 120 888 (Dar Es Salaam, Tanzania)

Wednesday, 23 December 2015

MASOGANGE AWAPIGA CHANGA LA MACHO WATU KUHUSU DAVIDO!

Agnes Masogange

Mwanadada muuza sura kiboko sana nchini Tanzania anayekwenda kwa jina la Agnes Masogange amekanusha kuwa na ujauzito wa msanii nguli wa muziki toka nchini Nigeria David Adedeji Adeleke ‘Davido’, akifungukia ishu hiyo bint huyo anayesifika kwa figa matata amesema “Hivi unajua mimi nashangaa sana kuhusu maneno ya mimi na Davido! Anawezaje sasa kunipa mimba jamani wakati hatuna uhusiano wa kimapenzi? Hiyo mimba inapitia wapi? Watu wanahisi tu kwamba nina uhusiano na Davido lakini siyo kweli na hakuna mwenye uhakika kuhusu hilo,” alisema Masogange.

David Adedeji Adeleke ‘Davido'

Pamoja nalo pia Masogange aliweka wazi kwamba yeye anamtu wake anayeshirikiana nae kimapenzi na siyo Davido. Licha ya Masogange kunanusha habari hiyo lakini dawati la Kachumbari lina data zenye uhakika kwamba Masogange anatoka kimapenzi na Davido. Tusubiri tuone!

No comments:

Post a Comment