wembe ads

wembe ads

Search Posts

Tanzania's Number one gossip blog with latest entertainment news, scandals, fashion and videos. contacts +255 789 120 888 (Dar Es Salaam, Tanzania)

Monday, 11 January 2016


MATUKIO YALIYOJIRI NDOA YA WASTARA


Msanii wa filamu hapa nchini Wastara Juma amefunga ndoa kwa mara nyingine na Mh. Mbunge wa Jimbo la Donge, Zanzibar, Sadifa Juma iliyofungwa Alhamisi iliyopita, kuna matukio ya kustaajabisha.

Ndoa hiyo iliyofungwa kimyakimya, ilifanyika mwishoni mwa wiki iliyopita nyumbani kwa mwigizaji huyo, Tabata-Barakuda, jijini Dar ambapo ilihudhuriwa na watu wachache tofauti na ilivyotarajiwa kutokana na umaarufu wa wanandoa hao.



NDOA ILIFUNGWA KWA SIMU
Imebainika kuwa, awali ndoa hiyo ilikuwa ifungwe saa kumi jioni na baadaye kuelezwa ilisogezwa mbele hadi saa 12 jioni, hata hivyo haikufungwa muda huo baada ya bibi harusi kuchelewa kufika akitokea saluni alikoenda kupambwa na kulazimika shehe afungishe ndoa hiyo kwenye simu wakati Wastara akiwa kwenye foleni barabarani. 

BWANA HARUSI AGOMA KUPIGWA PICHA
Imeelezwa kuwa, baada ya bwana harusi kutinga na wapambe wake alitoa onyo kali huku likisisitizwa na wapambe wake kuwa hairuhusiwi kupiga picha na kutuma kwenye mtandao wowote wa kijamii kwa vile ndoa hiyo ilikuwa ya siri. 

                                    AGOMA KUMFUNUA BIBI HARUSI
Katika hali ya kushangaza, baada ya bibi harusi kuwasili aliingizwa katika chumba maalum kwa ajili ya kumsubiri mumewe na hata alipoingia ndani, shehe alimuomba amfunue mkewe ili kumhakikisha kama ndiye yeye kitu ambacho alikipinga na kudai hakuwa na shaka naye na kuomba waendelee na kitu kingine.

No comments:

Post a Comment