Msanii asoishiwa vituko ndani ya Bongo movies na Bongoflavour Baby Madaha amevunjika mguu chanzo kikidaiwa kujidunga ulabu mpaka kuwa njwiii! Baada ya kumaliza kugonga vyombo na vikakolea kichwani akaelekea nyumbani kwake ambako baadaya kuingia chooni aliteleza na kuanguka. Baada ya tukio hilo aliwahishwa hospital ambako madaktari walimwambia kwamba amevunjika mguu na kisha kuwekewa P.O.P. Dawati la Kachumbari lilipomtwangia baby Madaha ili kujua ukweli alikiri na kusema anauomba mungu amponye kwa haraka ili arejee kwenye mishe mishe zake. Tunamtakia "Quick recovery" Baby Madaha ili aendeleze libeneke!
No comments:
Post a Comment