wembe ads

wembe ads

Search Posts

Tanzania's Number one gossip blog with latest entertainment news, scandals, fashion and videos. contacts +255 789 120 888 (Dar Es Salaam, Tanzania)

Tuesday, 26 January 2016

MAMA IDRIS AIKANA MIMBA YA WEMA!




Mama mzazi wa mshindi wa shindano la Biga Brother Africa mwaka 2015 / 2016 Idris Sultan amesema hautambui unaosemwa kuwa ni ujauzito wa msanii chakaramo wa Bongo Movies ambaye pia aliwahi kuwa Miss Tanzania mwaka 2006 /2007 Wema Sepetu mpaka pale atakapoongozana na Wema kwenda kumuona daktari ili apimwe na ithibitike!


SHILOLE AJILIWAZA SOUTH AFRIKA BAADA YA KIBUTI!




Msanii machachari wa muziki wa kizazi kipya Shilole ametamba kwenye mitandao ya jamii kwamba sasa ni mwenye furaha baada ya ku-break up na aliyekuwa mpenzi wake Nuh Mziwanda. Shilole alijinasibu kwamba sasa ana mpenzi mpya na ameamua kujipa faraja mwenyewe nchini Afrika kusini ili afungue ukurasa mpya.

LINAH AMWAGWA NA KAKA YAKE ZARI!



Ni rasmi sasa mwanamuziki wa bongoflavour Linah Sanga amemwagwa na aliyekuwa mpenzi wake Sebugeme, ingawa bado lina anaficha ukweli wa sababu ya kumwagwa kwake na pia mpenzi wake huyo kukana kuzungumzia habari hiyo lakini habari zenye uhakika zinadai kwamba mwanaume huyo alifikia uamuzi huo baada ya kugundua kwamba Linah hajatua.

RICHARD KIBOKO KABISA!



Aliyekuwa mshindi wa shindano la Big Brother Africa season 2 ambae kwa sasa anafanya maisha yake nchini Canada Richard Bezuidenhout amejibu mapigo baada ya mkewe kutishia kuivunja ndoa yake kutokana na kile kilichodaiwa kusambaa kwa picha chafu zinazoashiria uwepo wa mahusiano kati ya mshindi huyo wa zamani wa shindano la big Brother Africa pamoja na wanawake kadhaa. Richard ambae pia ni bonge la msanii wa filamu aliyewahi kuwika hapa nchini na filamu kibao ameamua krudisha majeshi yaani kuondoka nchini humo na kurejea hapa nchini Tanzania. Richard amekaririwa akisema kwamba ameona bora aonyeshe kwa vitendo kile kilicho kilichopelekea mgoror katika ndoa yake. Akifafanua hilo Rich alisema ameamua kurudisha majeshi hapa nchini ili kuendelea na shughuli zake za filamu ili watanzania waone uwezo wake ulivyokuwa akimaanisha ni tofauti na hapo awali ambapo alikuwa akiigiza bila taaluma ya fani hiyo ambapo kwa kuanzia ameshakamilisha filamu ya Kiswahili nchini Canada inayokwenda kwa jina la “Mwanaume siyo ATM Machine” ambayo inatarajia kusambazwa hapa nchini Tanzania hivi karibu.

Friday, 15 January 2016

HUDDAH ANAMBEMENDA HARMONISE!


Baada ya kuibuka kwa penzi kati ya mlimbwende Huddah Monroe wa Kenya na msanii chipukizi wa Tanzania Harmonise, wadau wengi wamedai kwamba mlimbwende huyo anambemenda mtoto huyo mwana bongoflavour zao la Diamond Platnumz! hayo yanasemwa pia kutokana na kukomaa kwa matendo ya mlimbwende Huddah kwenye historia yake ya mahusiano ya kimapenzi na kote alikopita ikiwa inaaminika kwamba harmonise ni kifaranga tu kwa mlimbwende huyo.

BOND AMLILIA WASTARA!

Msanii wa filamu hapa nchini Bond bin Sinani aliydumu kwenye mahusiano ya kimapenzi na msanii mwenzake Wastara Juma kwa muda mrefu, hivi karibuni alimwaga machozi kumlilia mpenzi wake huyo baada ya kuolewa ndoa ya ghafla. akizungumzia tukio hilo Bond alisema ameumizwa sana na kitendo cha Wastara kuamua kufunga ndoa kwa siri na ghafla bila kumfahamisha.

Kidoa akiwa na Mbwana Samatta
 Video Queen Asha Salum ‘Kidoa” amenaswa akijiachia kimapenzi na star bingwa wa mpira barani Afrika Mbwana Samatta. Wawili hao wamenaswa  juzikati wakiwa katika hoteli ya Girafe iliyopo maeneo ya Mbezi beach jijini Dar Es Salaam.